SIASA ZA KITAIFA




kinara wa chama cha wiper kalonzo musyoka amesema kwamba ana imani kuwa kwa ushirikiano na viongozi wengine watambandua afisini rais dkt william ruto

kwa kushinda uchaguzi mkuu wa mwaka 2027.

akiongea kwenye eneo bunge la likoni katika kaunti ya mombasa, kalonzo

ameusuta uongozi wa rais ruto akisema kwamba umefeli kushughulikia

maslahi ya wananchi kama walivyokuwa wameahidi.

kalonzo ameongeza kwamba sekta muhimu kama vile afya na elimu zimeendelea

kukumbwa na changamoto kutokana na sera mbovu zilizoanzishwa na serikali

ya kenya kwanza baada ya kutwaa mamlaka ya nchi.

Insert kalonzo on ukombozi.

 

KITAIFA

viongozi kwenye chama cha odm wameendelea kukariri kwamba chama hicho hakijaingia katika serikali ya kenya kwanza kufuatia kuteuliwa kwa baadhi ya wanachama wake kama mawaziri.

mbunge wa suba kaskazini millie odhiambo amesema kwamba chama hicho

kinaendeleza ushirikiano na serikali kwa ajili ya kuboresha utendajikazi kwa

manufaa ya wananchi.

kulingana na odhiambo ambaye ni kiranja wa walio wachache bungeni ni

kwamba kufikia sasa hakuna mkataba wa kuingia serikalini uliotiwa saini baina ya chama cha chungwa na utawala wa kenya kwanza.

Insert odhiambo on serikali..

 

 

 

 

BUNGOMA

maafisa wa usalama kwenye eneo la bungoma kaskazini wameimarisha msako dhidi ya watu majambazi waliomwangamiza mlinzi wa shule ya upili ya

namboko wiki iliyopita.

akiongea kwenye mkutano wa kiusalama mkuu wa polisi eneo hilo sammy

kosgei hata hivyo amewahimiza wananchi kushirikiana na maafisa wa usalama kwa kutoa taarifa muhimu.

kosgei amesema kuwa taarifa kutoka kwa wananchi utasaidia katika

kufanikisha uchunguzi utakaosaidia kuwabaini waliohusika na mauwaji ya

kinyama ya mlinzi huyo.

Insert kosgei on usalama

aidha naibu kamishna eneo hilo martin mureithi amekariri kwamba

watahakikisha waliohusika na mauwaji ya mlinzi huyo wanakamatwa na

kuchukuliwa hatua za kisheria.

Insert mureithi on washukiwa

 

trans nzoia

jumla ya shule tano za msingi katika kaunti ya trans nzoia zinatarajiwa kufaidi na vitabu vya kusoma vilivyotolewa kupitia kwa ufadhili wa wahisahi kutoka

kwenye kundi la giants group of nairobi twiga.

akiongea baada ya kupokea vitabu hivyo vyenye dhamani ya shilingi milioni

mbili, gavana george natembeya amesema kwamba ufadhili huo utairamisha uwezo wa wanafunzi kusoma na hivyo kuimarika kimasomo.

aidha kwa upande wao wahisahi hao akiwamo mkuu wa kundi hilo nakesh besai na mkewe chetna besai, wamewataka wazazi kuhakikisha kwamba wanao

wanasoma wakati wako nyumbani kando na kuzingatia nidhamu.

Insert natembeya on kusoma.

 

 

POKOT MAGHARIBI

gavana wa kaunti ya pokot magharibi simon kachapin ametangaza kuwa

wafanyabishara wanaoendesha shughuli zao katika soko la bendera eneo la kapenguria hawatahitajika kulipa ushuru kwa mwaka moja.

akiongea kwenye hafla ya ufunguzi wa soko hilo, gavana kachapin amesema

hatua hiyo itahakikisha wafanyabishara hao wanajimudu mwanzo kabla ya kuanza kulipa kodi.

aidha gavana kachapin ameahidi kwamba utawala wake utaendelea kuimarisha mazingira ya biashara kwa afanyabishara ili kuwapa nafasi ya kuendeleza shughuli zao bila changamoto.

Insertt kachapin on kodi

 

KIMATAFA.

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu ametishia kujitoa kwenye makubaliano ya kusitisha mapigano katika Ukanda wa Gaza.

Netanyahu ameyaagiza majeshi yake kujiandaa kuanzisha tena mashambulizi dhidi ya Hamas ikiwa hawatawaachia mateka zaidi siku ya Jumamosi.

Hamas ilisema siku ya Jumatatu na kurudia jana Jumanne kwamba pengine watasogeza mbele muda wa kuwaachilia mateka watatu wa Israel wakiishutumu kwa kushindwa kukidhi masharti ya makubaliano ya kusitisha mapigano.

Rais Donald Trump wa Marekani baada ya kukutana na Mfalme Abdullah II wa Jordan kwenye Ikulu ya White House siku Jumanne, alielezea mashaka yake ikiwa Hamas watawaachilia mateka wote waliosalia kama ambavyo amekuwa akishinikiza.

 



 

 

Show quoted text

Comments

Popular posts from this blog

mawakili wa kukodishwa KAUNTI ya trans nzoia